Udukuzi umekuwa ukihatarisha vifaa vya kidijitali na kusababisha watu kuwa na hofu kuwa na vitu vya kidigitali kwa hofu ya kudukiwa kwa vifaa hivyo.
Smart Tv ni kifaa mojawapo cha kiditali ambacho kimekuwa cha kuvutia sana kutokana na vitu ambavyo unaweza ukiwa na Smart TV.
Kwa mfano mbali na kwamba unaweza kufanya vyote ambavyo unaweza kufanya ukiwa na TV kutoka kampuni ya LG, Samsung, Sony(ambazo sio Smart TV), Smart TV ni mbadala wa computer aina ya Desktop kwani kwenye Smart Tv unaweza ukafanya chocohote ambacho ingekuhitaji ukifanye kwa kwenye desktop(komputa ya mezani).
>Lakini kwanini uzuie Smart TV yako isidukuliwe?
Kuzuia wezi wasiingie ndani ya nyumba yako: Wadukuzi wanaweza kutumia sauti umeihifadhi ambayo intumika kama ufunguo wa nyumba yako.
Username na neno siri: Uwezekano wa wadukuzi kutumia username yako na password kuweza kuingia kwenye akaunti zako nyingine. Inashauriwa kutotumia neno siri linalofanana katika akaunti zako.
Kushare kifaa chako na kompyuta nyingine: Kama utakuwa umeshare Smart Tv yako na kompyuta nyingine basi kompyuta hizo nazo zitakuwa katika hatari ya kuduliwa kutokana na kuwa shared na kompyuta nyingine.
>Kitu cha kufanya kuepuka kudukuliwa kwa Smart TV
- Kuwa na masasisho yaliyotoka. Smart Tv ni kifaa ambacho kinatakiwa kiwe na masasisho ya wakati huo wakati wote hivyo basi inatakiwa kuhakikisha masasisho zinakuwa installed pale zinapokuwepo. Njia hii itaongeza ugumu kudukua kifaa hicho.
- Kuhakikisha unaweka nyilwa kwenye mtandao wa smart Tv. Ni muhimu kuweka neno siri amabalo sio rahisi kufikirika katika network ya Smart TV ili kuifanya iwe salama na kutodukuliwa.
- Kuzima kamera. iwapo Smart TV yako ina kamera hakikisha unaizima baada ya kuitumia kuzuia kudukuliwa.
- Kuwa makini na ujumbe ambao unapokea. Unaweza ukapokea ujumbe ambao hauna maana hivyo unatakiwa kuwa makini na ujumbe unapokea kupitia Smart TV yako.
- Kutoka mtandaoni. Ni muhimu kuhakikisha unazima intaneti kama hauitumii ili kuepusha kifaa chako kudukuliwa.
Tuandikie maoni yako kuhusu makala hii kwa kuacha comment yako nasi tutajibu. Fuatilia TeknoKona katika Instagram, Facebook na Twitter.
Vyanzo: AllClearID, Tech times