Mtandao wa SMART ambao ni moja ya mtandao uliosambaza zaidi minara ya teknolojia ya 4G jijini Dar es Salaam umezidi kujiweka katika nafasi nzuri baada ya kuanzisha kifurushi cha 4G cha wiki bila kikomo.
Kwa shilingi 30,000/= za kitanzania basi utaweza kuperuzi kudownload chochote unachotaka kwa wiki nzima mchana na usiku, hii haina kiwango kwamba GB zako zimeisha hapana hii ni bila kikomo ushindwe wewe tu ama hiyo series unataka kudownload iishe.
Kifurushi hiki kinawafaa watu kama ambao tunapenda kupakua mafaili makubwa kutoka mtandaoni hata kama tumefulia, kwasababu hamna mtu anayetaka kulipa gharama kubwa katika kifurushi ambacho unaweza kukipata kwa bei naafuu na pia katika kasi kama ya SMART 4G.
Kujiunga na kifurushi hiki piga *149*00# na kisha unafuata maelekezo, mtandao huu ndio wanaongoza kwa kuifikisha intaneti yao ya kasi ya 4G katika maeneo mengi zaidi jijini Dar es salaam kama inavyoonekana katika picha hapo chini.
> http://tz.smarteastafrica.com/