Mataifa kadha wa kadha duniani yanapambana kupunguza kama si kuondokana kabisa na hewa chafu inayosababishwa na vitu mbalimbali, upo mpango wa kutengenza spika za masikioni zitakazokuwa na uwezo wa kuchuja hewa chafu.
Bara la Asia na kwa asilimia kubwa nchini Uchina inateseka sana na hewa chafu inayozalishwa kutoka kwenye viwanda, magari jambo ambalo linaweza kusababisha mtu akapata ungojwa wa kiharusi au saratani.
Katika kuja na kitu cha utofauti kabisa kampuni moja, Dyson ina mpango wa kutengeneza spika za masikioni ambazo tofauti na kufanya kazi ambayo inafahamika pia zitakuwa na uwezo wa kuchuja hewa chafu.
Spika hizo bado hajiaanza kutengenezwa lakini mapema mwaka huu Dyson walionekana wakipeleka mchoro ili kupata ithibati (patent) ya kile watakachokitengeneza.
Ubunifu na teknolojia kwa ujumla ambapo vinalenga kukabiliana na tatizo la hewa chafu ili kuepukana na madhara/vifo vinavyoweza kuzuilika.
Vyanzo: Engadget, CNET, Bloomberg