Mtandao maarufu duniani unaokuwezesha kutazama filamu, tv shows na vipindi vingine mbalimbali kupitia njia za kimtandao, Netflix, wawawezesha watumiaji wa huduma zake kutumia huduma hiyo ata pale watakapokuwa mbali na huduma za intaneti.
Netflix ni nini?
Netflix ni huduma namba moja duniani ya kukupatia video za filamu na tamthilia kwa njia ya kuzitazama kupitia huduma ya intaneti, kimombo ‘streaming’.
Je ni bure?
Hapana, kuna vifurushi kadhaa ila kifurushi cha kuanzia ni dola $7.99 (Takribani Tsh 17,504/= au Kes 816/=). – Kuifahamu zaidi huduma ya Netflix – Netflix ni nini?
Hali ilikuwa kabla ya maboresho haya mapya?
Kabla ya maboresho haya mapya watumiaji wa Netflix wa mtandao na wanaotumia app ya Netflix kwenye simu na tableti iliwabidi lazima wawe na huduma ya intaneti ili kuweza kutazama videos (streaming) za huduma hiyo.
Maboresho haya yanaleta nini hasa?
Huwezo wa kudownload filamu au show kwa ajili ya kuiangalia ata pale ambapo mtumiaji hatakuwa na intaneti umeletwa kwa watumiaji wa app ya Netflix kwenye simu na tableti tuu kwa sasa. Wakitangaza maboresho haya Netflix wamesema wanatambua kuna mazingira mengi huwa yanawakuta wateja wakiwa hawana huduma za intaneti za uhakika, mfano wanapokuwa safarini n.k.
Uwezo huo tayari unapatikana moja kwa moja kwenye app yao kwa watumiaji wote wa iOS na Android. Kutumia nenda kwenye app na kisha bofya eneo la ‘Available for Download’.