Mambo yanabadilika na vitu vipya vinatoka kila leo; sasa hata kama simu haipo katika kundi la kutambulika kama simu janja basi itakuwa na kamera kuifanya iweze kuvutia na kuuzika kwa watu/mataifa mbalimbali.
Mambo yalivyo hivi sasa simu janja ni lazima iwe na kamera angalau mbili ili kuweza kuwa katika nafasi nzuri ya kuwa katika usindani lakini bado ikaonekana hiyo haitoshi na siku hizi si kitu cha kushangaza kuona kamera 3-4 kwenye simu moja.
Mambo yapo mbioni kubadilika na kampuni, Light iliyojikita katika utengenezaji wa kamera ipo mbioni kuja na simu janja yake ambayo itakuwa na kamera 5-9 na kamera zote hizi zitakuwa kwenye simu moja.
Simu hii inaelezwa kuwa itakuwa na uwezo wa kupiga picha za ubora wa MP 64 bila kutumia kiasi kikubwa cha mwanga (flash).
Simu hii inaangaziwa kuja kuwa tishio na pengine kuongeza sababu kwanini zile kamera ambazo zilikuwa maarufu sana zikitumiwa kwa nadra sana tangu matumizi ya simu janja yashamiri.
Light wanafamika sana kwa bidhaa ya L16 (kamera 16 ndani ya kamera moja) ingawa kwa simu hii ambayo bado inatengenezwa inaonekana kuja kuifanya tena kampuni ikawa haabri ya muda mrefu vinywani mwa watu.
yazo: TechCrunch, The Verge, Hindustan Times