Wakati dunia ikifurahia ukuaji wa teknolojia kurahisisha mambo mengi lakini kwa upande mwingine imekuwa pigo na kilio kwa watu na hilo limewakumba mawakala katika sekta ya utalii kwa kupoteza kipato kutokana na ujio wa teknolojia.
Mawakala wa utalii nchini Kenya wanapoteza hadi asilimia 60 ya soko kutokana na kuwa watalii sasa wanajihifadhia nafasi katika maeneo wanayotaka kutalii kwa njia ya mitandao na simu.
Tafsiri yake ni shilingi za Kenya takribani 39 milioni kila mwaka hazipatikani kutokana na uwepo wa teknolojia. Kwa sasa, watumiaji wa intaneti nchini humo ni milioni 36.09 kulingana na mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya.