Kampuni ya Tidal ni moja kati ya makampuni maarufu sana duniani ambayo yanajihusisha na huduma ya ku’strem kazi za wasanii.
Mtandao huu ulinunuliwa na mwanamuziki Jay Z, baada ya kuununua alifanya maboresho mengi ambayo yaliweza kulikuza kampuni kwa ujumla. Lakini kumbuka bado kuna changamoto nyingi maana kuna washindani wakubwa kama vile Apple Music na Spotify.
Jambo la kubadilisha CEO katika kampuni kubwa kama hili linaleta taswira mbaya kwa ujumla, Wakuu wakiondoka na kuliacha kampuni mara nyingi inaonekana kuwa kampuni halifanyi kazi vizuri au halifikii malengo kwa wakati.
Aliekua CEO, Bw. Jeff Toig ameondoka katika kampuni hii ya Tidal. Mara ya kwanza kabisa CEO huyu alitoka katika mtandao wa ku’stream wa SoundCloud.
Huyu ni CEO wa tatu kuondoka katika kampuni hilo ndani ya kipindi cha miaka miwili. Awali Bw. Andy Chen na Peter Tonstad waliliacha kampuni na kuondoka — hao wakaenda zao — kwingine.
“Moja kati ya sababu ambazo zinatufanya tuendelea kukua zaidi, TIDAL tutatangaza CEO mpya katika wiki za hivi karibuni. Lakini kwa upande mwingie tunamtakia mema aliekua CEO wetu Bw. Jeff Tog popote aendapo” —- Walisema Tidal.
Ripoti zilizopo zinasema kuwa CEO huyo aliondoka mwezi Machi baada tuu ya Tidal kupata dili la uwekezaji la dola milioni 200 kutoka Sprint.
Kumbuka pia bado kampuni halifanyi vizuri kwa upande wa watu ambao wame’subscribe’ katika mtandao huo. Tidal waliweka wazi kuwa wana ‘subcribers’ milioni moja tuu. Hii ni namba ndogo sana ukilinganisha na Apple Music au hata Spotify.
Kwa namna moja au nyingine kampuni inabidi lifanye juu chini katika kuhakikisha kuwa linajikuza kwa kiasi kikubwa ili kuleta ushindani na makampuni mengine.