Tweet ya aliyekuwa Rais wa Marekani Barak Obama inayohusu kuvumiliana ndio tweet iliyopendwa (Like) zaidi katika historia ya Twitter.
Tweet hiyo ambayo ni ya kwanza kati ya tatu zinazomnukuu Nelson Mandela na liliandamana na picha ya Rais Obama aliyekuwa akitabasamu na kundi moja la watoto wa rangi tofauti.
Imependwa zaidi ya mara milioni 3 tangu ilipochapishwa mnamo tarehe 13 mwezi Agosti kufuatia shambulio la Charlottesville Virginia.
Tweet ya Obama inazidi kuendelea kupokea Likes..angalau hapa chini
“No one is born hating another person because of the color of his skin or his background or his religion…” pic.twitter.com/InZ58zkoAm
— Barack Obama (@BarackObama) August 13, 2017
Tweet hiyo imeipita ile ya Ariana Grande alipotuma salamu za rambirambi baada ya shambulio la kigaidi la Manchester ‘Taught to Love'{Nilifunzwa kupenda}.
Katika tweet hizo tatu kwenye akaunti yake ya Twitter, Bwana Obama alinukuu mshororo mmoja katika kitabu cha wasifu wa Mandela, The long Walk to Freedom.
”Hakuna aliyezaliwa akimchukia mwengine kwa sababu ya rangi mizizi yake ama hata dini”.
Nukuu hiyo ilisema: Watu wanafaa kujifunza kuchukia, na iwapo wanaweza kujifunza kuchukia pia wanaweza kufunzwa kupenda kwa kuwa mapenzi huja yenyewe katika moyo wa binaadamu kinyume na chuki.
Picha hiyo inaonyesha ziara ya bwana Obama 2011 katika kituo cha kuangalia watoto katika eneo la Bethesda, mjini Maryland.