Mtandao wa The Verge umeripoti kwamba tarehe 19/09/2016 Twitter itafanya maboresho mengine ambayo tayari yalikwisha tangazwa mwezi Mei, pamoja na yote mtandao huu sasa hautahesabia viambatanisho vilivyo ndani ya tweet katika hesabu ya tarakimu 140.
kwa sasa majina, picha, video, GIF ama link hazitahesabiwa katika tarakimu 140 ambazo mtu anaruhusiwa kutumia katika tweet moja, maboresho haya yanalenga katika kuwaruhusu watumiaji kujieleza kwa urahisi zaidi katika mtandao huu.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba @Twitter wameongeza uwezo wa watu kuandika tweets kwa kuondoa viambatanisho kama picha video GIF na vinginevyo katika hesabu ya tarakimu 140, hii inamaanisha kwamba sasa tunaweza kushiriki mijadala mbalimbali kwa ufasaha bila kujibana.
Yafuatayo ni mabadiliko mengine ambayo yanatarajiwa kuja mwezi huu…….
1. .@ Kwa sasa haitatumika tena!
Sio kila mtu alikuwa anaijua na kuitumia hii .@ ????(mimi ni mmoja wa watu ambao walikuwa hawaitumii) ni kwamba kwa sasa ukiandika tweets ukaanzia na jina la mtumiaji mfano @Teknokona basi tweet hii itamfikia @Teknokona pekee ila wanaokufuata hawataiona ilikua ukitaka wengine waione basi lazima uanze na nukta.
Twitter wanataka kubadili hili hivyo siku zijazo Tweets zote zinazo anza na jina la mtumiaji zitaweza kuwafikia watu wote wanaomfuata mtumiaji.
2. Majina pia hayata hesabiwa!
Kwa sasa ukitweet basi majina ya wale ambao unawapelekea ujumbe huo pia yanahesabiwa, hili ni moja kati ya mambo ambayo yatabadilishwa mwezi huu na hivyo majina yatakuwa hayahesabiwi.
One Comment
Comments are closed.