Mtandao wa kijamii ya Twitter umetangaza kupiga marufuku matangazo ya sarafu za kidigitali (Cryptocurrency) na kuanzia jumanne hakutakuwa na matangazo ya sarafu hizo katika mtandao wake.
Uamuzi kama huu tayari umeshachukuliwa na makampuni mengine kadhaa ya huduma za matangazo ya mtandaoni kama vile Google, na Facebook. Sababu kuu ambayo imetolewa na mitandao hiyo ni kwamba hatua hii inawasaidia kuwalinda watumiaji wa huduma zao dhidi ya udanganyifu au hasara inayoweza kutokea kwa kujihusisha na biashara hii.
Katika soko la mtandaoni, kuna sarafu 1587 za kidigitali ambazo ‘huchimbwa’ na kugeuzwa pesa halisi. Mifano ni Bitcoin, Ethereum, Ripple, Bitcoin Cash, LITECOIN na Cardano.
Marufuku hiyo inahusu ofa ya kwanza ya sarafu (ICOs) na mauzo, ilisema kampuni hiyo wakati wa mahojiano na Reuters Jumatatu.
Kampuni hiyo imepiga marufuku pia biashara za kampuni za sarafu hizo kutangaza biashara zao ikiwa hazijaorodheshwa katika soko la hisa linalofahamika.