Watu 21 wamekamatwa kwa kuwalaghai maelfu ya watu kupitia mitandaoni na kuwaibia kiasi kikubwa cha fedha nchini Uchina.
Kwa mujibu wa shirika la Sinhua, watu zaidi ya 20 chini ya jina la jukwaa la uwekezaji wa intaneti, walidanganya watu kwa kuwaahidi kuwa watapata kipato zaidi. Watu hao 21 wamejipatia kipato kinyume na sheria cha takribani $132 milioni kupitia mtandaoni.
Watuhumiwa wametajwa kuwa na umri kati ya miaka 16 na 20 wamekuwa wakiiba fedha za watu kupitia katika tovuti za manunuzi ya mitandaoni na imebainika wamefanya uhalifu kwenye takribani majimbo 12 ya Uchina.
Imeelezwa kuwa polisi wa Uchina walianza ufuatiliaji wa kiufundi na kuweza kubaini jukwaa la ulaghai mwezi Desemba 2017. Baada ya miezi 6 ya ufuatiliaji wa kiufundi uliofanyika Guangdong, Ciangshi, Ciciang na Guangxi Cuang watu hao 21 wamepatikana na kukamatwa.
Taarifa haijaweka wazi ni tovuti gani hasa iliyotumika kuwaibia watu lakini imebainika kuwa tovuti waliyokuwa wanaitumia ilikuwa katika mji wa Linyi ulioko katika jimbo la Shandong Mashariki mwa Uchina na iliweza kuchukua saa 2 na nusu kwa mtu kuweza kuibiwa kiasi cha fedha katika akaunti yake.