Tunatumia simu, kompyuta, memori za ziada, n.k lakini vitu vyote hivyo zipo vina ukubwa wa ambao ukitathmiini ni namba shufwa tu ndio zinakuwa zimebeba kifaa husika.
Kila swali lina jibu au majibu kulingana na mada/kipengele husika na pengine wewe ni kati yale ambao wakati fulani walishawahi kujiuliza “Kwanini simu, memori ya ziada, kompyuta ukiangalia ukubwa wake upo kwenye kundi la namba shufwa?”. Jibu lipo tena lakini ni muhimu kukumbushana kidogo.
Namba shufwa ni namba yoyote inayogwanyika kwa mbili (2) bila kubaki. Hapa ndio utavuta taswira kuwa vifaa vyetu vya kidijiti (vilivyo na uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu) ukubwa ambao umbo kwenye kundi hilo la namba; GB 8, GB 16, GB 32 na kuendelea.
Ukweli kuhusu namba shufwa kwenye vifaa vya kutunza kumbukumbu.
Kompyuta, rununu, kifaa cha kidijiti vinatafsiri chochote katika ufanyaji wake wa kazi ni mfumo wa sifuri na moja (0/1) ikimaanisha 2^n (n=namba yoyote nzima kuanzia sifuri). Sasa basi kwenye kwa sababu namba zilizokamilika zipo zinambulika kama 0/1 basi hesabu kamili inaweza kuwa kama ifuatavyo:-
2^0 = 1
2^1 = 2
2^2 = 4
2^3 = 8
2^4 = 16
.
.
.
.
Sasa kama kifaa husika kina ukubwa wa GB 128 hiyo inakuwa ni sawa na kama inavyoonekana pichani.