Tafiti za Cisco imeonyesha uwezekanano wa vifaa vinavyotumia iOS na Mac kudukuliwa kwa kutumia file lililo katika mfumo wa picha la lenye kirusi.
Utafiti huo umebainisha kuwa file lililo katika mfumo wa TIFF linaweza likatumwa kwa njia ya MMS, barua pepe au likawekwa kwenye tovuti fulani halafu mtu akaongozwa kutembelea tovuti hiyo. Mbaya zaidi ni kwamba file hilo lina uwezo wa kuficha virusi na kuathiri kifaa chako bila kujua.
Aidha udhaifu huo unampa uwezo mdukuzi kuweza akafanya kila kitu hata akiwa mbali na kifaa hicho iwapo anakuwa ameweza kudukua kifaa chako; iwapo ameweza kupata password na username yako unayotumia na hivyo kuweza kupata idhini ya kuona na kufanya kila kitu kwenye kompyuta/iPad.
Tayari wahusika wamesharekebisha udhaifu huo ambao uliibuliwa na mtafiti kutoka Cisco na ili kifaa chako kiweze kuwa katika usalama inabidi kufanya masasisho ya programu endeshaji kuja kwenye toleo la karibu kwenye vifaa vyote kutoka Apple.
Ni matumaini yetu makala hii itakusaidia ili kuweza kuzuia kifaa chako kisidukuliwe. Kama kawaida yetu TeknoKona tupo na wewe kiteknolojia zaidi.
Vyanzo: TechJuice, EveningStandard, TnW