Wanasayansi waliweka vifaa vya kupima tetemeko la ardhi katika uwanja wa Nou Camp na kufanikiwa kupima mitetemeko ya ardhi kila nyota wa timu ya Barcelona, Lionel Messi anapofunga goli.
Wakati Lionel Messi anapofunga goli mji wa Barcelona hutetemeka na athari ya mabao yake huonekana katika data kila wakati mashabiki wanaposheherekea kwa kuruka juu na chini uwanjani.
Vipimo hivyo vilidhihirika wakati Barcelona ilipofanya miujiza ya kutoka nyuma na kuishinda klabu ya Paris Saint Germain katika kombe la klabu bingwa Ulaya msimu uliopita.
Tetemeko la ardhi linalosababishwa na kandanda limejadiliwa katika kongamano la sayansi la Ulaya huko Vienna, Austria. Ni kazi ya Jordi Diaz na wenzake katika taasisi ya sayansi ya ardhini.
Bw. Diaz na wenzake walibaini kuwa hata kwenye matamasha makubwa ya muziki mathalani tamasha la Bruce “The Boss” Springsteen au U2 yaliyowahi kufanyika katika uwanja wa Nou Camp yana uwezo wa kulitikisa jiji zima la Barcelona.