Je haupendi aina ya mwandiko uliopo katika app ya WhatsApp? Usihofu, WhatsApp wapo njiani kuleta aina mpya ya muonekano wa herufi zake (font style) na muda wowote kuanzia sasa utaweza kuzitumia.
Maboresho haya yameshaonekana katika matoleo ya WhatsApp yaliyo katika matengenezo, yaani ‘Beta’.
Aina ya font utakayoweza tumia inafahamika kwa jina la FixedSys na unaiweza kuiona kupitia kompyuta yako ya Windows au ata kwa kutafuta Google.
Tatizo kuu ni jinsi ya kuitumia, inaonekana kama WhatsApp hawatatafuta njia rahisi kabisa ya font hiyo kutumika basi inawezekana wengi wakaona ni kazi kweli kuitumia mara kwa mara. Kuweza kutuma ujumbe katika muonekano huo inabidi unapoandika uweke alama tatu za kufungua na kufunga semi – mwanzoni na mwishoni…yaani ‘. Mfano – ”’UJUMBE WAKO”’
Kwa sasa uwezo huo upo katika toleo la beta, toleo namba 2.16.179 kwa Android na pia ata kwa iOS tayari lishaanza lishaanza kuonekana kwa watumiaji wa WhatsApp beta.
Ukiacha hili pia inasemekana WhatsApp wapo njiani kuleta uwezo wa kutumia video fupi za mfumo wa GIF na pia uwezo wa kupiga na kupokea simu katika mfumo wa video.
Soma Pia
- Jinsi ya kuweka Bold, tide na Italic kwenye Whatsapp
- Idadi Ya Simu Zinazopigwa Kwa Siku kwa Kutumia app ya WhatsApp!
- WhatsApp Gold? – Epuka meseji hizi, zitakuwekea virusi kwenye simu
- WhatsApp wapo njiani kuleta WhatsApp Video Call: Piga simu za Video
Endelea kutembelea mtandao wako wa TeknoKona kwa habari na maujanja mbalimbali ya Teknolojia!
Vyanzo: Na mitandao mbalimbali