Kampuni ya simu za Xiaomi imetangaza kufungua duka la simu zake katika uwanja wa ndege wa Shenzhen Baoan nchini China jumamosi ya machi 10, 2018.
Xiaomi katika kipindi cha nyuma ilizingatia kwenye maduka ya mtandaoni zaidi kuliko maduka halisi ya kawaida na yaliyozoeleka.
Hata hivyo Xiaomi ilibadilika kwa kuanza kufungua maduka ya kawaida ya kuuzia simu zake. Hadi sasa ina mamia ya maduka iliyofungua katika nchi kadhaa duniani.
Aidha sambamba na duka hilo la uwanja wa ndege Xiaomi itafungua maduka mengine katika sehemu mbalimbali kama Changsha Wanjiali shop, Jiaozuo Wanda Plaza shop, Jinzhou beautiful future shop, Yu City, na Peak City Square store.