Miamala kwa njia ya simu ni jambo la kawaida sana katika nchi nyingi tu za Afrika na huduma za M-Pesa na TigoPesa zinazotolewa na Tigo na Vodacom Tanzania zimepewa vyeti kuidhinishwa kuwa huduma bora za kifedha.
HUduma za kifedha zinatumika sana na kuwa ajira kwa wengine, kurahisisha miamala (kutuma/kupokea pesa) na hata kuongea pato la taifa kwa njia ya ulipaji kodi. Mwaka 2018 Aprili 13 utaingia kwenye historia ya Tigo na Vodacom Tanzania baada ya huduma ya TigoPesa na M-Pesa kutimiza vigezo vyote kwa asilimia 100 hivyo kutambulika kimataifa kama huduma bora.
Undani wa TigoPesa na M-Pesa kupewa cheti cha ubora.
Katika kukidhi viwango vya mtoa huduma za kifedha anayetambika na GSMA Mobile Money ni laziam awe amechunguzwa na kuthibitika ni za kuaminika, kuna uwazi na usalama wa fedha za wateja wao. Vigezo vyote hivyo ni lazima mtoa huduma apate alama 100 katika kila kigezo kilichowekwa na GSMA Mobile Money.
Makampuni mengine yaliyopata cheti cha ubora kutoka GSMA Mobile Money ni pamoja na Orange Côte d’Ivoire, Safaricom (Kenya) na Telenor Microfinance Bank Ltd. (Easypaisa Pakistan).
2 Comments
Comments are closed.