Baada ya utafiti uliodumu kwa miaka 10, taasisi ya Sayansi ya kilimo nchini Uchina imeweza kukuza mpunga wa aina mpya ambao una urefu wa kufikia mita 2.2.
Kwa mujibu wa taasisi ya kisayansi ya Institute of Subtropical Agriculture (ISA) imesema mpunga huo mpya utazalisha mchele mwingi tofauti na mpunga ulizoeleka. Kwa kawaida mpunga wa kawaida huwa na urefu wa mita 0.9 hadi mita moja.
Shamba maalum lilitengwa kwa ajili ya ufaiti huo lilikuwa katika mji wa kaunti ya Changsha, katika jimbo la Hunan nchini Uchina. Mtafiti wa idara hiyo Bw. Xia Xinjie amesema kuwa mpunga huo unafanya usanisinuru kwa ufanisi mkubwa zaidi kuliko mpunga wa kawaida kwa asilimia 50.
Kwa wastani mmea mmoja una machaka 40, mpunga unaokua kwenye chaka moja unaweza kufikia zaidi ya 500, na uzalishaji wa michele unaweza kufikia tani 12 kwa hekta.
Bw. Xia amesema mpunga huo umekuwa wenyewe kwa kutumia teknolojia mbalimbali mpya zikiwemo kuchochea mabadiliko ya mpunga, kukuza mpunga chotara kwa kutumia mpunga pori, na kuchagua aina nzuri za mpunga kwa mujibu wa alama za molekuli.