Hupaswi kufikiria sana pale unaposikia kwa mfano kulipuka kwa betri za simu aina ya Lithium-ion kwani ni jambo ambalo lipo tamati kumalizika.
Tatizo la betri hizo zikiwamo zile zilizoleta shida wakati fulani kwenye Samsung Galaxy Note 7 limesababisha milipuko kadhaa mpaka maamuzi yakatoletewa kusitisha matumizi ya simu hizo na kuondolewa kabisa sokoni.
Hitilafu ya betri za Lithium-ion kulipuka limekuwa moja ya janga kubwa kwa baadhi ya simu tukio ambalo linaweza kusababisha vifo na wengine kupata majeraha kutokana na milipuko huo.
Baadhi ya watafiti wamekuja na toleo jipya la betri za Lithium-ion ambazo wanasema kuwa kamwe hazitashika moto kirahisi kwa maana ya kwamba betri hizo zitaendelea kufanya kazi hata kama itakuwa na tatizo kidogo.