Tecno ni moja kati bidhaa (simu janja) zilizoenea barani Afrika kwa wingi na kufanya kuwa na soko zuri barani humo lakini halikadhalika Tigo Tanzania nao wamekuwa wakijidhatiti ili kuweza kuendelea kufanya vizuri katika soko lenye ushindani na hatimae wasipoteze wateja.
Sote tunafahamu jinsi gani Tigo Tanzania ilivyokuwa na wateja wengi na kuzidi kuendelea kuwavutia watu wengine kila siku. Hivi karibuni Tigo Tanzania na Tecno wamua kushirikiana kwa faida ya wao na wateja wa bidhaa zao.
Siunafahamu simu janja mpya ya Tecno Camon X? Basi Tecno na Tigo Tanzania wanasema kwa kila mteja atakayenunua simu hiyo atakuwa anapata GB 3 za kifurushi cha intaneti BURE kila mwezi kwa muda wa miezi sita.
Ambacho pengine hukifahamu……
Tecno wameamua kufanya kazi na Tigo Tanzania kwa sababu ya Tigo kuwa na intaneti ya 4G katika maeneo mengi nchini humo (Tanzania) na isitoshe simu ya Tecno Camon X ina mfumo wa 4G hivyo kufanya wateja wake kufurahia intaneti yenye kasi kutoka Tigo Tanzania.
Tigo Tanzania ndio kampuni ya ya kwanza ya mawasiliano kuweza kuleta simu hizo katika maduka yake yote yaliyopo katika mikoa mbalimbali nchini Tanzania. Vilevile, mteja anaweza kununua simu janja ya Tecno Camon X kwa kulipa kidogo kidogo; unapiga *147*00# kisha utafuata maelekezo au kununua kupitia MTANDAONI.
Tecno Camon X inauzwa Tsh. 469,999 katika maduka yote ya Tigo ambapo simu hiyo itakuwa na kifurushi cha GB 3 za bure kila mwezi kwa siku 180. Bofya HAPA kujua sifa ya simu hiyo pamoja na mengineyo.
Chanzo: Tigo Tanzania