Vita ya kibiashara iliyoanzishwa na rais wa Marekani imesababisha Uchina kufikiria namna ya kupunguza kutegemea bidhaa za zinazotengenezwa kutoka kwenye taifa linaloongoza kiuchumi.
Uchina sasa imeamua kujifunga mkanda na kuamua kutengeneza vipuri ambavyo mizizi yake ni kutoka kwa AMD (processor) za 32 Bit ambazo zitafamika kama Dhyana.
AMD haiwatengenezei Uchina kisha kuwauzia bali imewaruhusu kutengeneza za vipuri hivyo vinavyotumika kwenye kompyuta kulingana na mahitaji ya nchi yao.
Mwaka 2015, Marekani ilizuia Intel pamoja na makampuni mengine yanayotengeneza vipuri vya kwenye kompyuta kwa sababu ya kuamini vitu hivyo vilikuwa vinachagiza Uchina katika utengenezaji wa silaha hatarishi sana (nuclear).
Uamuzi wa AMD unaweza kufanya kazi na Uchina kunaleta maana kwamba sasa upinzani mkali upo mbioni kurudi ambao ulionekana kupotea kwa miaka kadhaa.
Vyanzo: Techspot, Hexus