Data za wateja wa benki kuu ya Thailand (BOT) zimedukuliwa katika matawi mawili makubwa ya kibiashara na wadukuzi ambao hawajajulikana mpaka sasa.
Kulingana na shirika la habari la Sinhua, benki za ‘Kasikorn bank’ na ‘Krung Thai Bank’ zimethibitisha kuwa data za wateja zaidi ya 120 elfu zimeibiwa.
Wakati wataalam wa usalama wa mitandaoni kutoka benki kuu ya Thailand (BOT) wameahidi kuongeza hatua ulinzi wa taarifa za watu mitandaoni, watendaji wa benki zilizoathiriwa na udukuzi wamedai kuwa hawakuona dalili zozote za wizi wakati data hizo zikidukuliwa.
Wezi hao wametumia mbinu za kisasa kupata taarifa za wateja zaidi ya mia moja na ishirini elfu kisha kutumia taarifa hizo kuomba mikopo kupitia mtandao.