Apple ipo mbioni kuleta simu tofauti na zile ambazo ulimwengu imezoea kuziona; simu ambazo zitakuwa na uwezo wa kukunja na kujikunjua 🙄 🙄 🙄 .
Mpango wa Apple kutengeneza simu janja ambazo zina uwezo wa kukunja na kukunjua umekuwepo kwa miaka kadhaa sasa lakini taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika zinasema tutegemee kuona simu hizo mwaka 2020.
Simu hizo za Apple ambazo LG kazi yake ni kutengeza kioo/display ya OLED chenye uwezo wa kujikunja na kuweza kutumika kama simu janja au tabiti (tablet).
Apple ambao kwa miaka yote hawajawahi kuthubutu kutengeneza simu rununu ambayo itakuwa na uwezo wa kujikunja na kujikunjua wameonekana wakifanya kazi na washirika wake kutoka bara la Asia katika kufanikisha ujio wa simu hizo.
Je, hakuna makampuni ambayo yameshatengeza simu za kujikunja/kujikunua?
LG na Samsung wameshatengeneza simu janja za mfumo huu (simu kuwa simu janja au tabiti) lakini hakuna hata mmoja kati yao ambae ameziweka simu hizo sokoni.
Apple inafanyia kazi matoleo matatu yajayo kwa mwaka 2018 ya iPhone X ambayo mbili kati ya hizo kuja na vioo vya OLED na nyingine kuwa na kioo cha LCD. Usitegemee kuona teknolojia ya TouchID kwenye matoleo yanayokuja ya iPhone X; simu zote 3 zitakuwa na teknolojia ya FaceID yenye kamera ya hali ya juu.
SIfa na bei ya simu hizo za Apple zenye uwezo wa kujikunja na kujikunjua havijawekwa wazi lakini inawezekana ikawa ndio mwazo wa kuona makampuni mengine nayo yakitoa za kwao za muundo huo. Tutaendelea kufuatilia suala hili kwa ukaribu na kuwahabarisha.
The Verge, Gadgets 360
One Comment
Comments are closed.